Quantcast
Channel: HABARI NA MATUKIO
Viewing all 11654 articles
Browse latest View live

FIRST NATIONAL BANK YAFUNGUA TAWI MWANZA

$
0
0
Mkuu wa Biashara FNB Tanzania, Francois Botha akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella jinzsi mashine ya kisasa ya kuolea fedha inavyofanya kazi baada ya mkuu wa mkoa kuzindua huduma za benki hiyo jijini Mwanza.
---
Benki ya First National Bank Tanzania (FNB) imeendelea kupanua wigo kitaifa kwa kufungua tawi jipya eneo la Rock City Mall jijini Mwanza leo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, Mkuu wa Biashara wa benki hiyo, Francois Botha alisema uzinduzi wa tawi la FNB Mwanza umelenga kukidhi ongezeko kubwa la mahitaji ya huduma za kibenki na za kifedha katika mkoa huo.

“Uzinduzi wa tawi la Mwanza ni sehemu ya uwekezaji endelevu na mkakati wa kuhakikisha maeneo mengi ya nchi yanapata huduma bora za kifedha. Pia tumezingatia ukuaji wa haraka wa mkoa wa Mwanzaambao una mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Tanzania.”

Botha alisema tawi Mwanza ni la tisa miongoni mwa mtandao wa matawi ya FNB Tanzania ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa kupanua mtandao wa matawi ili kuyafikia maeneo yote nchini.

“ First National Bank daima tunafikiri njia mbalimbali za ambazo tunaweza kutoa huduma za kibenki kwa urahisi kwa wateja wetu. Tawi letu la Mwanza litatoa ufumbuzi wa kina kwa wateja wanao ishi Mwanza na maeneo jirani yenye biashara inayokua kwa kasi” Botha alisema.

Mara kwa mara tunafikiria mbinu mpya za kutuwezesha kutoa huduma inayowapa unafuu wateja wetu kwa kupeleka huduma hiyo karibu na makazi pamoja na biashara zao. Tawi hili litarahisisha huduma kwa wateja wetu wanaoishi jijini Mwanza na maeneo ya jirani ambayo yana biashara nyingi zinazokua kwa kasi,” alisema Botha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alisema mkoa wa Mwanza una uwezo mkubwa wa kiuchumi na ukuaji mkubwa wa sekta mbalimbali za kiuchumii karibuni ni ishara kuwa Mwanza inakua kwa kasi.

"Tunakaribisha uwepo wa FNB na tunatazamia kuwasaidia kuimarisha huduma zenu hapa na mikoa mengine," alisema Mkuu wa Mkoa.

Alisema mbali na mkoa wa Mwanza kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi wa nchi bali pia inazalisha mali nyingi na ina utajiri mkubwa wa rasilimali. “Tunatarajia kuwa mtatoa mchango mkubwa katika utoaji huduma za kifedha mkoani Mwanza kupitia huduma zenu mbalimbali kwa kutumia ubunifu na utaalamu wenu,” Mongella alisema.

Tawi hilo lililofunguliwa kwenye jingo jipya la Rock City Mall litatoa huduma za kawaida za kibenki pamoja na huduma za dijitali kwa masaa 24 ili mahususi kukidhi mahitaji ya watumiaji huduma pamoja na wafanyabiashara katika eneo hilo.

MJASIRIAMALI ALIYEWEZESHWA NA AIRTEL FURSA AISHUKURU AIRTEL

$
0
0
 Kijana mjasiriamali Diana Moshi (kulia) akimkabidhi keki Mkurugenzi wa kitengo cha Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano Mallya (kushoto) kama shukrani yake kwa Airtel baada ya kuwezeshwa kupitia mpango wa Airtel FURSA "Tunakuwezesha" kwa kukabidhiwa vifaa vya kisasa vilivyomsaidia kuboresha biashara yake ya kupika keki na kumsaidia kupata mafanikio. Makabidhiano hayo yalifanyika katika makao makuu ya ofisi za Airtel Morocco jijini Dar es Salaam.

NAIBU WAZIRI ANGELINA MABULA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA NHC

$
0
0
001 
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Mabula akifungua rasmi mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye makao makuu ya shirika hilo Upanga jijini Dar es salaam ambapo alilipongeza shirika hilo kwa kazi nzuri ambayo wafanyakazi wake wanaifanya kwani ndiyo shirika pekee la Serikali linaloendeshwa kwa ufanisi mkubwa na kuiletea heshima serikali, Waziri Mabula amewaambia wafanyakazi wa shirika hilo pamoja na Menejimenti yake kuendelea na kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya ili kuleta maendeleo zaidi nchini katika sekta ya nyumba. PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM
5 Mkurugenzi wa Shirika hilo Bw. Nehemia Mchechu akizunguma na wafanyakazi wa shirika hilo kabla ya Waziri Angelina Mabula kuufungua rasmi.
7 
Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Nyumba wakifuatilia mkutano huo.
8Wafanyakazi wa shirika la Nyumba wakiimba wimbo wa wafanyakazi kabla ya kufunguliwa kwa mkutano huo.
9Wafanyakazi wa shirika la Nyumba wakiwa katika mkutano huo.
11 Mkurugenzi wa Shirika hilo Bw. Nehemia Mchechu na Naibu Waziri Angelina Mabula wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa shirika hilo baada ya kuufungua rasmi mkutano huo.
12 Mkurugenzi wa Shirika hilo Bw. Nehemia Mchechu na Naibu Waziri Angelina Mabula wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa shirika hilo baada ya kuufungua rasmi mkutano huo.

RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA JENGO LA KITEGA UCHUMI LA MFUKO WA PENSHENI PPF JIJINI ARUSHA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akikata utepe kuzindua rasmi, Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni (PPF) lililopo Mtaa wa Korido Jijini Arusha leo Mei 9, 2016. Wa pili (kushoto) ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Mhe. Jenister Mhagama, (kushoto) ni Meya wa jiji la Arusha, Calist Lazaro (wa kwanza kutoka kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PPF, Ramadhan Kijjah, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango. Picha zote na Mafoto Blog
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio, baada ya kuweka Jiwe la Msingi la uzinduai wa Jengo la Kitegauchumi la Mfuko huo lililopo Mtaa wa Korido Jijini Arusha leo Mei 9, 2016.
Jengo hilo lililozinduliwa leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akihutubia wakazi wa arusha na wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakati alipozindua rasmi, Jengo la Kitegauchumi la Mfuko huo (PPF) lililopo Mtaa wa Korido Jijini Arusha leo Mei 9, 2016.
Sehemu ya wadau kutoka NSSF waliohudhuria uzinduzi huo wa wenzao wa PPF.
Sehemu ya wadau wakimsikiliza Mhe. Rais Dkt. Magufuli.....
Baadhi ya wafanyakazi wa PPF Kanda yas Arusha wakimsikiliza Mhe Rais wakati akihutubia.
Sehemu ya wananchi wa Jiji la Arusha wakimsikiliza Mhe. Rais Dkt. Magufuli.....
Wananchi wakimshangilia Mhe Rais wakati akihutubia.....
Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Mhe Rais.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakimsikiliza Mhe Rais wakati akihutubia.
Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni PPF na Wakurugenzi wa Mfuko wa huo wakimsikiliza Mhe Rais wakati akihutubia.
Baadhi ya viongozi na wadau wa Mfuko huo na Meya wa Jiji la Arusha Calist Lazaro (kushoto) wakimsikiliza Mhe Rais.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi PPF, Ramadhan Kijjah, wakati alipowasili kwenye Viwanja vya Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni PPF lililopo Mtaa wa Korido jijini Arusha kwa ajili ya uzinduzi wa jengo hilo leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio, wakati alipowasili kwenye Viwanja vya Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni PPF lililopo Mtaa wa Korido jijini Arusha kwa ajili ya uzinduzi wa jengo hilo leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akisalimiana na baadhi
ya Wadau wa Mfuko wa Pensheni PPF, wakati alipowasili kwenye Viwanja vya Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni PPF lililopo Mtaa wa Korido jijini Arusha kwa ajili ya uzinduzi wa jengo hilo leo.
Wakifurahia baada ya uzinduzi huo....
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akisalimiana na Meneja wa PPF Kanda ya Arusha, Onesmo Ruhasha, wakati alipowasili kwenye Viwanja vya Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni PPF lililopo Mtaa wa Korido jijini Arusha kwa ajili ya uzinduzi wa jengo hilo leo.
Picha ya pamoja baada ya uzinduzi huo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akisalimiana na Meneja Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele, wakati alipowasili kwenye Viwanja vya Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni PPF lililopo Mtaa wa Korido jijini Arusha kwa ajili ya uzinduzi wa jengo hilo leo.
Picha ya pamoja baada ya uzinduzi huo.
Viongozi wakiwa meza kuu wakiimba wimbo wa Taifa
Wadau wakiimba wimbo wa Taifa.
Wadau wakiimba wimbo wa Taifa.

TANZIA UK DIASPORA GLASGOW.

$
0
0
Tunasikitika kuwatangazia msiba wa Mtanzania mwenzetu 
Bi Mwasaburi Haji
kilichotokea Jumamosi jioni huko Glasgow Scotland.

Mipango ya mazishi inaendelea na mtajulishwa tarehe ya mazishi.
Msiba uko nyumbani kwa Marehemu
2/1, 105 Mcculloch St. Glasgow, G41 1NT.

Kwa wale mlioguswa mnaweza kutuma rambi rambi zenu kwenye account ya
ndugu wa marehemu 
A. AZIZ.
Nationwide.
Account No: 01491791
Sort code: 07 04 36.
Kwa mawasiliano zaidi mnaweza kumpigia ndugu wa Marehemu
A. AZIZ - 07411445644

Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Rajiun.

MAMA YAKE TEDDY MAPUNDA MAREHEMU BENADETTE IZENGO AZIKWA MAKABURI YA KINONDONI DAR

$
0
0
001
Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanania Dk. Gharib Bilal (wa tatu kutoka kushotona) Mama Salma Kikwete (kwanza kushoto) wakishiriki mazishi ya marehemu Benadette Izengo mama wa Mkurugenzi wa kampuni ya Montage Limited, Teddy Mapunda aliyekaa katikati yao pamoja na wanafamilia wengine wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam mara baada ya ibada iliyofanyika kwenye kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph.
01
Mke wa Rais Mstaafu Dk Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete akiweka mchanga kaburini wakati aliposhiriki mazishi ya Marehemu Mama Benadette Izengo yaliyofanyika jana kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
02 
Balozi Asha Rose Migiro akiweka mchanga kaburini wakati wa maishi ya marehemu mama Benadette Izengo.
1 
 Padre Matumaini akiongoza ibada ya mazishi ya Marehemu Mama Benadette Izengo iliyofanyika kwenye kanisa la Mtakatifu Joseph jana.
2Wanafamilia wakiwa katika ibada ya mazishi iliyofanyika kwenye kanisa la Mtakatifu Joseph jana jijini Dar es salaam na kufuatiwa na mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Kinondoni.
3 
Teddy Mapunda na Ndugu yake wakiwa pembeni mwa jeneza la mama yao mpendwa marehemu Benadette Izengo.
4 
 Mkwe wa Marehemu mama Benadette Izengo akishiriki ibada ya mazishi pamoja na ndugu na jamaa wa familia kwenye kanisa la Mtakatifu Joseph jana.
5 
 Wajukuu wa marehemu wakishiriki ibada hiyo jana.
6 
 Wana familia wakiwa na majonzi kwa kuondokewa na mpendwa mama yao Marehemu Mama Benadette Izengo.
7Mwenyekiti wa Chama cha UDP, Mzee John Cheyo akishiriki sakramenti ya bwana kutoka kwa Padre Kaombwe wakati wa ibada hiyo ya mazishi.
8 
 Teddy Mapunda na Mumewe Nestor Mapunda wakiwa na majonzi huku wakiangalia jeneza la mama yao mpendwa marehemu mama Benadette Izengo.
9 
 Baadhi ya waombolezaji wakishiriki mazishi kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
10 
Kutoka kushoto ni Joseph Kusaga Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Entertainment, Nandi Mwiyombela, Justin Pamba, Godfrey Kusaga na John Mbele nao walishiriki katika mazishi hayo ya mama Bebadette Izengo.

KAMISHNA MSAIDIZI KITENGO CHA HAKI ZA MTOTO AFUNGUA NYUMBA ZA KUNDI LA WATOTO WANAOELEKEA UJANANI KATIKA KITUO CHA MANAI CENTER MJINI MOSHI

$
0
0
Kaimu Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za kundi la watoto wanaoelekea ujanani katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Jengo jipya lililojengwa kwa ufadhili wa Emirates National Bank of Dubai (ENBD) kwa ajili ya watoto wanaoelekea ujanani katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akimuonesha Kaimu Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo maeneo mbalimbali ya jengo hilo katika ramani.
Moja ya muonekano wa chumba katika jengo hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi rasmi wa jengo hilo.
Baadhi ya walimu na walezi wa watoto katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center wakifuatilia shughuli mbalimbali katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akiteta jambo na Kaimu Kamishna kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo wakati wa hafla ya ufunguzi wa jengo hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akimkaribisha Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ,Agnes Urassa katika Hafla hiyo.
Baadhi ya watoto wanaolelewa katika kituo cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Kaimu Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa nyumba kwa ajili ya watoto wanaoelekea ujanani wa kituo cha kulelea watoto cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Mwakilishi wa Benki ya ENBD ambao wamefadhili mradi wa ujenzi wa nyumba hiyo,Fatma Rahman akizungumza katika hafla hiyo.
Mratibu wa miradi katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center,Jafary Salum akisoma taarifa ya ujenzi wa mradi huo.
Wawakilishi wa Benki ya ENBD ,Rhea Fernandes na Fatma Rahman wakionesha zawadi waliyotoa kwa watoto waishio katika kituo hicho.
Kikundi cha Sarakasi kinachundwa na watoto kikionesha umahiri katika mchezo huo.
Kaimu Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo akionesha umahiri wake katika kucheza Kwaito.
Wawakilishi wa Benki ya ENBD ,Rhea Fernandes na Fatma Rahman wakiondosha vitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba hiyo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WASEMAVYO WANANCHI; NGUVU ITUMIKAYO KUKAMATA WAHUJUMU UCHUMI WA SUKARI ITUMIKE KUPAMBANA NA MAJANGIRI

$
0
0
NGUVU ITUMIKAYO KUKAMATA WAHUJUMU UCHUMI WA SUKARI, endapo kama ingetumika kupambana na majangiri na waharamia wa wanyama pori, basi kwa hakika tungeweza kuokoa zaidi ya Tembo 90,000 waliouawa katika kipindi kimoja tu cha awamu ya serikali ya 4, kwa ajili ya biashara haramu ya pembe za ndovu!

Kwa sasa kg1 ya pembe za ndovu inathaminishwa kuwa ni TSh 4.5 Mill. na ikiwa kama pembe 1 ya ndovu inawastani wa kg30 basi itagharimu takribani Millioni 135 za Tz, ambapo fedha hiyo ni sawasawa na tani 750 za sukari iliyofichwa, na pia kama ni pembe zote 2 za tembo mmoja aliyeuawa basi itakuwa sawa na tani 1,500 za sukari, inayoweza kubebwa kwenye malori 50 yenye kontena kubwa za futi 40 kwa kila lori moja.

Mpaka hapo hoja yangu ni kwamba, katika kipindi cha miaka 10 iliyopita Tanzania tulipoteza zaidi ya Tembo 90,000 ambapo kwa wastani wa kila saa moja inakadiriwa kuwa Tembo mmoja aliuawa na maharamia hao haramu!! Kwa takwimu hizi, binafsi naona hii ni zaidi ya wahujumu sukari, ambapo kukamatwa na tani 4,500 za sukari ni sawa na Tembo watatu tu kati ya hao Tembo 90 elfu waliouawa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita!

Mdau,
Emmanuel Seni - Mtwara.

U.S. EMBASSY HONORS 2016 INTERNATIONAL WOMEN OF COURAGE LAUREATE MS. VICKY NTETEMA

$
0
0
U.S. Ambassador Mark B. Childress, Deputy Permanent Secretary Amon Mpanju from the Ministry of Constitutional and Legal Affairs, and the Executive Director of Under the Same Sun Tanzania, Vicky Ntetema, hold the 2016 International Women of Courage award after a ceremony held at U.S. Embassy Dar es Salaam. The ceremony was also attended by other Tanzanian government officials and civil society advocates and leaders. Ms. Ntetema originally received the award from Secretary of State John Kerry on March 29 at a ceremony in Washington. (Photo Courtesy of U.S. Embassy)
Musician Sixmund Mdeka (singing) performs during the 2016 International Women of Courage award ceremony held at the U.S. Embassy Dar es Salaam to honor Vicky Ntetema, the Executive Director of Under the Same Sun Tanzania. The ceremony was also attended by U.S. Ambassador Mark B. Childress and Deputy Permanent Secretary Amon Mpanju from the Ministry of Constitutional and Legal Affairs, as well as other Tanzanian Government officials and civil society stakeholders. Ms. Ntetema originally received the award from Secretary of State John Kerry on March 29 at a ceremony in Washington. (Photo Courtesy of U.S. Embassy)
---
U.S. Embassy Dar es Salaam today honored Vicky Ntetema, Executive Director of Under the Same Sun Tanzania, as a recipient of the 2016 International Women of Courage award. Ms. Ntetema originally received the award from Secretary of State John Kerry on March 29 at a ceremony in Washington.

The ceremony at the U.S. Embassy was attended by Mr. Amon Mpanju, Deputy Permanent Secretary of the Ministry of Constitutional and Legal Affairs, as well as other Tanzanian government officials and civil society advocates and leaders.

In his remarks, Ambassador Childress lauded Ms. Ntetema’s advocacy, saying “We stand here today with our international partners and Government of Tanzania partners committed to ending these attacks because they are a gross violation of basic human rights and because persons with albinism have the right to be free from fear in their own homes.”

During the ceremony, Vicky Ntetema said “I urge the police in Tanzania to work with their colleagues in Interpol to further investigate these killings and expose cross-border trade of People With Albinism (PWA) organs and trafficking.”

Dedicating the award to PWA and their families, Ms. Ntetema specified that, “This prestigious award is for all persons with albinism. It is for babies, children, women and men who felt every inch of the machete attack as death stared in their faces; It is for all those who have added physical disability to their low vision, just because witchdoctors ordered their body parts for a client; The award is for those without albinism who have been forced to leave their homes and villages in order to protect their loved ones with albinism; and for those who live in constant fear because they witnessed the macabre killings and know that the murderers would recognize them.”

Giving his remarks, Deputy Permanent Secretary Amon Mpanju from the Ministry of Constitutional and Legal Affairs said that, “The government will continue to ensure security of our people, including those with disabilities, and this is a joint work and not only the work of the government. We need support from the media people to do investigative journalism on the attacks of people with albinism, and also from communities who live with people with disabilities. The government will work together with justice stakeholders to ensure that these people with disabilities access their rights. The target is to see this killings come to an end.”

Vicky Ntetema is Tanzania Executive Director of Under the Same Sun, an NGO dedicated to ending the discrimination and violent attacks against people with albinism. A decade ago, as the BBC’s Tanzania Bureau Chief, Ms. Ntetema went undercover to investigate the illicit business of buying and selling the body parts of people with albinism. Posing as a potential buyer, she infiltrated networks of witchdoctors who claimed the body parts could bring luck to purchasers. Death threats followed the airing of Ms. Ntetema’s stories, and temporarily forced her into hiding. But her courageous reporting galvanized international attention and led to a series of arrests and convictions. Ms. Ntetema has remained fearless, eventually leaving journalism to fight with international public and private sector partners for the human rights of people with albinism.

Established in 2007, the annual Secretary of State's International Women of Courage Award honors women around the globe who have exemplified exceptional courage and leadership in advocating for human rights, women’s equality, and social progress, often at great personal risk. This is the only Department of State award that pays tribute to emerging women leaders worldwide.

MBUNGE WA DODOMA MJINI NA NAIBU WAZIRI WA KAZI, VIJANA NA AJIRA, MHE. ANTONY MAVUNDE ATEMBELEA KAMBI TIBA YA GSM DODOMA

$
0
0
 Na Mwandishi Wetu

Mbunge wa Dodoma Mjini na Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde leo amefanya ziara ya kushtukiza katika kambi tiba ya GSM Foundation inayofanywa na kikosi cha Madaktari bingwa kutoka hospitali ya MOI, ambayo kuanzia leo imepiga kambi Dodoma baada ya kutoka katika mikoa ya Mwanza, Singida, na Shinyanga.

Akieleza sababu za kuitembelea kambi hiyo ambayo iko katika hatua zake za mwisho kumaliza awamu ya kwanza, Mheshimiwa Mavunde amebainisha kwamba kwanza, ni kwa sababu alisikia kambi iko katika jimbo lake, lakini jingine kubwa na la msingi likawa ni kupeleka shukrani zake kwa Maafisa wa Taasisi ya GSM wanaoambatana na madaktari kuweka kambi tiba hizo katika kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa na vichwa vikubwa na migongo wazi kila mwaka.

"Nimeshtushwa na takwimu za mwaka juzi, kwamba wanaozaliwa ni 4000 na wanaorudi hospitali kwa ajili ya tiba hawazidi 600. Hii ni hatari, ilipaswa mtu kuchukua jukumu la haraka na nimeshukuru kusikia GSM mmefanya hilo, hongereni sana", alisema Mavunde.

Mavunde amewataja Maafisa wa GSM na Madaktari kuwa ni watu wenye moyo wa kizalendo ambao wanatakiwa kuigwa na jamii, wameacha familia zao, na wameamua kuokoa maisha ya watoto ambao hata hawawajui, kwa sababu moja tu kubwa na ya msingi ya utanzania.

PICHANI JUU: Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde(Wa Pili kutoka kulia) akikaribishwa eneo la Hospitali na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bw Jordan Rugimana(Wa tatu kutoka kulia) na Naibu Mkurugenzi wa MOI ambaye ndio mratibu wa kambi tiba ya GSM DK Othman KIloloma(Wa nne kutoka kulia) na Meneja wa Taasisi ya GSM BI Shannon Kiwamba(kushoto)
Mh Mavunde akisikiliza maelezo ya mmoja kati ya wagonjwa waliohudhuria kambi tiba ya GSM
 Mratibu wa Kambi Tiba ya GSM, Dk Othman Kiloloma akimpa taarifa za wagonjwa Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde ambaye pia ni Mbunge wa Dodoma mjini
 Mh Mavunde akiongea na wanahabari waliokuwa hospitalini hapo kufuatilia habari za wagonjwa waliohudhuria kambi tiba ya GSM
Mh Mavunde akibadilishana mawazo na mratibu wa kambi tiba ya GSM, Dk Othman Kiloloma, wanaosikiliza ni Kibwana Matukio kutoka GSM, na Mganga mkuu wa mkoa Bw Jordan Rugimbana.

WARAMI WAMPONGEZA RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI KWA KUWATETEA WANYONGE, WASEMA ANAPIGWA VITA NDANI YA BUNGE NA NJE YA BUNGE

$
0
0
12 
John Marwa Mratibu wa Chama cha Watetezi wa Rasilimali Wasio na Mipaka WARAMI akizungumza na waandishi wa habari Kwenye Hoteli ya Tamarin Mwenge jijini Dar es salaam kuhusu Sakata la Sukari ambapo amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa jinsi anavyothubutu kuwatetea watanzania waliowanyonge katika masuala mbalimbali na hasa katika suala zima la uhaba wa sukari.

Kuna tani nyingi za sukari zimekamatwa katika msako maalum ambao Rais aliamrisha vyombo vya dola kufuatilia wafanyabiashara wasio waaminifu walioficha sukari, baada ya zoezi hilo kuanza sukari nyingi imeendelea kukamatwa maeneo mbalimbali nchini ikiwa imefichwa na baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu.
WARAMI inapongeza jitihada zote za dhati anazozifanya Rais Magufuli na Serikali yake za kuhakikisha watanzania wanaishi kwenye usawa, lakini pamoja na hayo wanapendekeza mambo kadhaa yafanyika na jeshi la polisi.

Mratibu huyo wa Taasisi ya WARAMI amelitaka jeshi la polisi kutoa taarifa rasmi juu ya wafanyabiashara wanaotamba barabarani kuwa wameliweka jeshi hilo mfukoni kwamba hakuna wa kuwafanya lolote katika nchi hii.
Taasisi za kiserikali zifafanue juu ya tabia hii ya wafanyabiashara kutumia picha za viongozi kwa maslahi yao kama, ni haki ama si haki.
Kiongozi huyo wa WARAMI akaongeza kwamba hivi sasa Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli anayo vita kubwa kutokana na kazi anayoifanya ya kuwatetea watanzania waliowanyonge anayo vita ndani ya bunge na nje ya Bunge.
Kutokana Na Hoja Ambazo Zimekuwa Zikitolewa Na Baadhi Ya Wabunge Zikikosoa Utendaji Wa Rais, kuna baadhi ya watu wamekuwa wakifaidika na baadhi ya mambo hivyo wasingependa mabadiliko ya kumkomboa mwananchi wa kawaida yatokee, katika picha kushoto ni Makdeo Makeja mratibu msaidizi WARAMI
 14 
Makdeo Makeja mratibu msaidizi WARAMI akifafanua jambo wakati viongozi hao wa taasisi ya WARAMI walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam , kulia ni John Marwa Mratibu wa Chama cha Watetezi wa Rasilimali Wasio na Mipaka WARAMI.

RAIS MSTAAFU, JAKAYA KIKWETE AKAGUA DARAJA LA NYERERE

$
0
0

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akipewa maelezo ya awali na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, alipokagua daraja hilo leo Mei 10, 2016. Kulia ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akionyeshwa barabara zinazopishana ya juu na ya chini, alipokagua daraja ya Nyerere, Dar es Salaam, leo Mei 10, 2016.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akiuliza jambo, alipokagua daraja la Nyerere, Dar es Salaam, leo Mei 10, 2016. Kushoto ni Mama Salma Kikwete.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembea kwenye daraja la Nyerere, Dar es Salaam, leo Mei 10, 2016, walipokagua daraja hilo.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akitazama moja ya ofisi zitakazotumiwa na magari kulipia ushuru wa kutumia daraja la Nyerere, alipokagua daraja hilo leo Mei 10, 2016. (Picha na Bashir Nkoromo).

DARAJA LA NYERERE KUANZA KULIPIWA JUMAMOSI MEI 14, 2016

$
0
0
Katibu mkuu: Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi Mhandisi Joseph Nyamhanga akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanza kutozwa kwa vyombo vya usafiri vitavyopita katika Daraja la Nyerere kuanzia jumamosi ya Mei 14.(Picha na Raymond Mushumbusi) MAELEZO
---
Na Raymond Mushumbusi - MAELEZO, DAR.

Serikali imetangaza rasmi kuanza kwa tozo kwa vyombo vya usafiri vitakavyopita katika daraja la Nyerere kuanzia Jumamosi tarehe 14 ,mwezi huu.Akizungumzia na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema kuwa kuanzia siku hiyo , vyombo vyote vya usafiri vitatakiwa kulipia ushuru wa kupita katika daraja la Nyerere.

“ Tumeanza kutoza tozo hii mara baada ya kufunguliwa kwa daraja hili na kuanza kutumika kwa kupita bila kulipa kwa vyombo vya usafiri tangu Aprili 19 mwaka huu na sasa tunaanza rasmi kutoza tozo kwa ajili ya kukusanya gharama za usimamizi, utunzaji na uendeshaji wa daraja hili.” alisema Mhandisi Nyamhanga.

Mhandisi Nyamhanga amefafanua kwamba watembea kwa miguu watapita bure katika daraja hilo huku wenye baiskeli wakilipia Sh. 300, pikipiki Sh. 600, waendesha maguta ,bajaji na magari ya kawaida (Saloon Cars) watatakiwa kulipia Sh.1500.Mabasi yanayobeba abiria 15 yatalipia Sh. 3,000, yale ya abiria zaidi ya 15 Sh. 5,000 na yale yanayobeba abiria zaidi ya 29 yatalipia Sh. 7,000.

Aidha magari yenye tani zaidi ya mbili mpaka saba yatalipia Sh. 7,000, tani 7 hadi 15 watalipa Sh.10,000, tani 15 mpaka 20 watalipa Sh.15,000 na yale yenye tani 20 mpaka 30 yatalipia Sh. 20,000.

Mhandisi Nyamhanga ameongeza kuwa magari yenye namba za Jeshi la Wananchi (JWTZ), Jeshi la Polisi (PT), Jeshi la Magereza (MT), gari za wagonjwa, magari ya zimamoto na magari yenye vibali maalum yataruhusiwa kupita bure.

NANI ALAUMIWE???? GARI LA POLISI LAGONGA GARI LA MWENDO KASI

$
0
0

MAADHIMISHO YA MIAKA SITA YA CHAMA CHA WATANZANIA WALIOSOMEA CHINA (CAAT)

$
0
0

Chama cha Watanzania Waliosoma China kwa kiingereza China Alumni Association of Tanzania (CAAT) kinapenda kukukaribisha katika sherehe ya maadhimisho ya miaka 6 (2010-2016) tokea kilipozaliwa.

Sherehe hiyo itafanyika katika ukumbi wa Cardinal Laurian Rugambwa Social Centre pembezoni mwa kanisa la Mtakatifu Peter (St Peter), Oysterbay Ijumaa ya tarehe 20-May-2016 kuanzia saa 8 alasiri.

Sherehe hiyo itahudhuriwa na viongozi wakubwa kutoka serikalini na baadhi ya wageni kutoka ubalozi wa China.

Pamoja na burudani mbalimbali, maadhimisho hayo yatakuwa na hotuba kutoka viongozi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na viongozi wa ubalozi wa Jamhuri ya watu wa China.

Kwenye sherehe hiyo pia utafanyika uzinduzi wa tovuti (website) ya CAAT. Baada ya chakula cha pamoja cha jioni, vilevile kutakuwa na fursa ya wafanyabiashara, wajasiliamali na wafanyakazi waajiriwa kuonyesha bidhaa au matangazo ya bidhaa au huduma wanazotoa.

Dhima kuu ya tukio hilo ni;

•Utambulisho wa jumuia ya CAAT ambayo inajumuisha wataalam wa taaluma mbalimbali waliohitimu mafunzo yao katika Jamhuri ya Watu wa China

•Kubaini na Kuainisha fursa zinazopatikana Tanzania na China kupitia CAAT

•Maonyesho ya bidhaa na huduma mbalimbali za biashara za wanajumuia.

Wote mliopata kusoma China mnakaribishwa. Hakutakuwa na kiingilio.

Unaweza kushiriki kwa kuthibitisha uwepo wako kwa kupiga simu kwa Katibu Mtendaji wa CAAT kwa kupitia 0783-992020 au 0715-200090 au email gsoreku@yahoo.com

Asante,
George Oreku
Katibu Mkuu
Chama cha Watanzania Waliosoma China (China Alumni Association of Tanzania)
05-May-2015

GREEN VOICES WASAIDIA KILIMO CHA UYOGA DAR

$
0
0
Bi. Esther Chiombola akionyesha uyoga ambao uko tayari kuvunwa. Uyoga huo unalimwa na kikundi cha Tunza Women Group cha Bunju jijini Dar es Salaam kwa ufadhili wa mradi wa Green Voices (Makala na Picha zimeandaliwa na www.brotherdanny.com).
Bi. Sauda Issa miaka 70 (kushoto) mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam akipokea zawadi ya kitabu maalum kinachozungumzia kilimo cha uyoga kutoka kwa Bi. Esther Chiombola ambaye ni Ofisa Kilimo Msaidizi Mwandamizi wa Manispaa ya Kinondoni.
Mratibu wa vikundi vya kilimo cha uyoga Bunju na Boko, Magdalena Bukuku (katikati) akiteta jambo na mratibu wa green Voices nchini Bi. Secelela Balisidya wakati wa uzinduzi wa mradi huo unaofadhiliwa na Green Voices. Wengine pichani kutoka kushoto ni Bi. Lucresia Tarimo aliyemwakilisha Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Kinondoni, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kilungule Seif Stambuli, na Ofisa Kilimo Kata ya Bunju, Rhoda Mruttu. 
Bi. Sophia Chove, mwenyekiti wa kikundi cha wakulima wa uyoga Bunju, akitoa maelekezo kwa watu mbalimbali kuhusu namna ya uchanganyaji wa vimeng’enyo vya kuoteshea na kukuzia uyoga. 
Mchanganyiko maalum wa vimeng’enyo vinavyotumika katika kilimo cha uyoga. 
Uyoga ukiwa unaoteshwa katika eneo maalum kwa kufunikwa kaniki. 
Mchuzi mzito wa uyoga ulioandaliwa kwa ajili ya chakula cha mchana. Uyoga huo umevunwa katika mradi wa kikundi cha akinamama wa Bunju chini ya ufadhili wa Green Voices. 
Wageni waalikwa wakishiriki chakula cha mchana ambacho mboga kuu ilikuwa uyoga. 
  Akinamama sita, ambao ni sehemu ya akinamama 15 ambao wanatekeleza mradi wa Green Voices baada ya kupatiwa mafunzo nchini Hispania mwanzoni mwa mwaka huu. Kutoka kushoto ni Siddy Abubakar Mgumia, Farida Hamisi, Tukuswiga Mwaisumbe, Secelela Balisidya, Magdalena Bukuku na Judica Losai.

RAIS DKT. MAGUFULI AWASILI NCHINI UGANDA KWA AJILI YA KUSHIRIKI TUKIO LA KUAPISHWA RAIS MTEULE WA UGANDA YOWERI KAGUTA MUSEVENI

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na mwenyeji wake Rais Mteule wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya maua kama ishara ya Ukaribisho kutoka kwa mtoto katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda mara baada ya kuwasili kutokea Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais Mteule wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni wakati nyimbo za mataifa mawili pamoja na ule wa Afrika Mashariki ukipigwa katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Maafisa mbalimbali waku wa vyombo vya Ulinzi wa Serikali ya nchini Uganda mara baada ya kuwasili nchini humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili katika Ikulu nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa heshima wakati akikagua gwaride rasmi la heshima mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kwenye kikundi cha ngoma za asili mara baada ya kuwasili kwenye Ikulu ya nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mwenyeji wake Rais Mteule wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha Pongezi wakati alipowasili katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kwenye kikundi cha ngoma mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Entebe nchini Uganda. PICHA NA IKULU

AFISA UTUMISHI MANISPAA YA ILALA ASIMAMISHWA KAZI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Paul Makonda, akizungumza na wakuu wa idara mbalimbali wa mkoa huo kuhusu kubainika kwa watumishi hewa wengine 39. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi na Mkuu wa Wilaya ya Temeke,Sophia Mjema. Picha zote na Elisa Shunda
---
JUMLA ya watumishi hewa wengine 39 wamebainika katika Mkoa wa Dar es Salaam ikiwa ni wiki moja tangu Mkuu wa Mkoa wa huo, Paul Makonda, kuwasainisha mikataba wakuu wa idara zote kuhusiana na watumishi hao. 

Imeelezwa kuwa hadi sasa watumishi hewa 248 wamebainika mkoani hapa na kuisababibishia serikali hasara ya takriban Sh.bilioni 3.6. 

Akizungumza na viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo maofisa utumishi, wakuu wa idara, wakurugenzi na wakuu wa wilaya jana jijini hapa, Makonda alisema watumishi hao 39 wameisababishia serikali hasara ya Sh. milioni 724.

Kufuatia sakata hilo, Makonda alimwagiza mkurugenzi wa Ilala, Isaya Mngurumi, kumwandikia barua ya kumsimamisha kazi Ofisa Utumishi wa manispaa hiyo, Francis Kilawe, kutokana na kubainika watumishi hewa 11 ambao licha ya kutoonekana katika idara zao, waliendelea kulipwa mishahara.

Alisema ili taifa liweze kupiga hatua, kila mmoja kwa nafasi aliyonayo hana budi kufanya kazi kwa bidii kumsaidia Rais John Magufuli katika kuhakikisha kuwa maendeleo yanapatikana.

Hata hivyo, akizungumzia suala hilo baada ya mkutano huo kuisha, Mngurumi alisema atamuomba Makonda kutengua adhabu ya ofisa huyo kwani tangu alipowasili kikazi katika manispaa hiyo, haizidi miezi miwili.

“Ofisa huyo ametoka Ilemela na kuja hapa, kwa hiyo nitazungumza na mkuu wa mkoa ili amuondolee adhabu hiyo kwa sababu hana muda mrefu tangu awasili hapa,”alisema.

Makonda alisema amewapa muda wa wiki mbili kwa wakuu hao wa idara kuwasaka watumishi hewa na baada ya hapo, kazi hiyo itakuwa endelevu kwa kila aliyepewa dhamana ya kuisimamia ili kuokoa fedha zilizokuwa zikipotea.

“Haiwezekani mkuu wa idara akae bila ya kufahamu namna ya kuifanya kazi yake hadi alazimishwe au asimamiwe, nataka kuona kila mtu akitekeleza jukumu lake alilopewa kikamilifu,”alisema.

Mkuu huyo wa mkoa alisema serikali imetenga Sh.bilioni 40 kwa ajili ya maendeleo, hivyo bila ya kuwepo na kasi ya utendaji kazi, fedha hizo zinaweza kuliwa na wajanja na hatimaye lengo lisipatikane.

Makonda amewataka viongozi husika kuchukua hatua stahiki dhidi ya watumishi hao ili fedha zilizopotea zirejeshwe pamoja na kufunguliwa mashtaka kwa waliobainika.

TIGO YATOA MSAADA WA VYANDARUA KWA HOSPITALI YA UKEREWE

$
0
0
Mkurugenzi wa Kanda ya ziwa wa mtandao wa tigo Ali Maswanya(fulana ya blue), akimkabidhi Vyandarua 80 Kaimu Mganga Mkuu wa  Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe Dk Kaniki Titus,kwenye hafla ya Makabidhiano iliyofanyika Mwanza juzi.
Mkurugenzi wa Mikakati (Director of Strategy) wa tigo Kobbina Awuah(wa tatu kushoto) akimkabidhi Vyandarua 80 Kaimu Mganga Mkuu wa  Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe Dk Kaniki Titus,kwenye hafla ya Makabidhiano iliyofanyika Mwanza juzi.

SERIKALI MKOANI MBEYA YAFUTA HATI YA KIWANJA CHA MAKAZI KILICHOTOLEWA NA HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makala (Picha Maktaba)

Na EmanuelMadafa,Mbeya(Jamiimojablogu).

SERIKALI Mkoani Mbeya imeagiza kufutwa kwa hati ya kiwanja kilichotolewa na halmashauri ya Jiji la Mbeya kwenye chanzo kikuu cha maji kilichopo eneo la Nyibuko kata ya Mwakibete kwa matumizi ya makazi.

Agizo hilo, limetolwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala mara baada ya kutembelea na kukagua chanzo kikuu cha maji cha Nzovwe, chenye uwezo wa kuzalisha mita 12 za ujazo kwa siku na kusambaza maji kwa asilimia 41 kwa wakazi wa jiji la Mbeya wapatao zaidi ya 200,000.

Kiwanja hicho ambacho kipo karibu na eneo la chanzo cha maji cha Nzovwe, kilitolewa na maafisa ardhi, idara ya mipango miji kwa ajili ya matumizi ya makazi na kumilikiwa na mtu binafsi aliyetajwa kwa jina moja la Mwakasala.

Makala amesema, chanzo hicho cha maji ndio tegemezi kwa kusambaza huduma ya maji kwa wananchi wa Jiji la Mbeya, hivyo kama kitaachwa na kuharibiwa, wananchi zaidi ya 200,000 wapo hatarini kuikosa huduma hiyo ambayo ni haki yao ya msingi.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Serikali iliwaondoa wananchi wote waliokuwa wanaishi au kuendesha shughuli zao za kiuchumi ndani ya mita 60 na kuwalipa fidia zao hivyo hatua ya wananchi hao kuendelea kuishia mahali hapo ni kukaidi agizo la serikali.

Amebainisha kuwa kiwango kikubwa cha upotevu wa maji kwa asilimia 31 inatokana na baadhi ya vyanzo vya maji kuharibiwa kwa kufanyika kwa shughuli za kibinadamu, kulisha mifugo au kujenga nyumba za makazi pamoja na mabadiliko ya kihaidrolojia.

Hata hivyo, Mkuu huyo aliutaka uongozi wa mamlaka ya maji kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa halmashauri ya Jiji la Mbeya, kuhakikisha wanalisiamamia zoezi hilo la kumondoa mvamizi huyo ndani ya siku tatu.

“Wananchi wengine wameondoka tena kwa hiari yao wenyewe, sasa kwa nini huyu atuchezee mchezo mchafu?.. kwa hili sikubaliani nalo, huku akiwataka wananchi ambao ni vijana kulilinda eneo hilo na kuwaonya wale ambao watakubali kutumiwa na mtu au watu kufanya fujo,”alisema.
Viewing all 11654 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>