Quantcast
Channel: HABARI NA MATUKIO
Viewing all 11654 articles
Browse latest View live

RAIS DKT. JOHN MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI TAREHE 03 MEI 2016 MKOANI DODOMA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri tarehe 03 Mei, 2016 katika ukumbi wa TAMISEMI mjini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein mara baada ya kutoka kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri tarehe 03 Mei, 2016 katika ukumbi wa TAMISEMI mjini Dodoma.PICHA NA IKULU

TAASISI YA MISAADA YA KIJAMII YA HAMISI KIGWANGALLA KUMSOMESHA GETRUDE CLEMENT

$
0
0
a32603a8-b5b0-41d7-8533-7baf03333277
Mwanzilishi wa Taasisi ya Misaada ya Kijamii ya Hamisi Kigwangalla, Naibu Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa katika picha moja na Getrude Clement ambaye atalipiwa ada ya kidato cha tano na cha sita.

Kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa kizazi cha miaka ijayo, Taasisi ya Misaada ya Kijamii ya Hamisi Kigwangalla iliyoanzishwa na Naibu Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla imejitolea kumlipia ada Getrude Clement kwa masomo yake ya kidato cha tano na sita.

Uamuzi huo wa kumsomesha Getrude umekuja baada ya leo kukaribishwa kuongea kwenye kikao cha wabunge watetezi wa haki za watoto ambapo Getrude alipata nafasi ya kutoa historia yake ambayo iliwatoa baadhi ya wabunge machozi.

Getrude aliwaeleza wabunge historia yake na hali yake ya kimaisha na kusema kuwa baba yake ni kinyozi na mama yake anafanya biashara ndogo ndogo za nyanya na vitunguu lakini bado amekuwa akijtuma katika masomo yake ambapo kwa sasa yupo kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Mnarani, Mwanza.

Baada ya kusema hivyo ndipo Dkt. Kigwangalla aliamua kujitoa kumsaidia mtoto huyo ili aweze kujiendeleza zaidi kielimu na kufikia malengo yake na zaidi akiahidi kumsomesha katika shule za kisasa ili apate elimu bora zaidi.
ce18d8f2-cd50-4b46-8193-3351745537ac
“Kwa kuthamini kipaji chake na mchango wake na kutambua nafasi yangu kama Naibu Waziri kwenye Wizara inayosimamia mambo ya Watoto na kama mbunge na mzazi wa mabinti, lakini zaidi kama mtu kutoka kwenye background ya maisha ya chini na ninayethamini mchango wa elimu kwenye maisha yangu, nimeamua kujitolea kumsomesha kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa,

“Taasisi yangu ya misaada ya kijamii ya Hamisi Kigwangalla Development Foundation itamlipia ada za masomo yake ya high school,” alisema Dkt. Kigwangalla.

Getrude Clement ambaye ana miaka 16 amepata nafasi hiyo ya kipekee baada ya kupata nafasi ya kutoa hotuba kwa niaba ya watoto na vijana wengine duniani katika mkutano wa Umoja wa Mataifa ambapo alikaribishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na kusifiwa na watu mbalimbali duniani kutokana na hotuba yake nzuri.

RAIS DKT. MAGUFULI ASHIRIKI KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM MKOANI DODOMA

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiendesha Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa kilichofanyika Mkoani Dodoma. Kulia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kushoto ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein wakifurahia jambo kabla ya kuanza kwa kikao cha cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa kilichofanyika Mkoani Dodoma.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati alipowasili mkoani Dodoma kwa ajili ya kikao hicho cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakielekea kwenye kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa kilichofanyika Mkoani Dodoma. PICHA NA IKULU.

MAMIA WAJITOKEZA KUMUAGA 'KAMANDA' GABRIEL MWAIBALE

$
0
0
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Gabriel Peter Mwaibale aliyefariki juzi nyumbani kwao Mabibo jijini Dar es Salaam ambapo mazishi yake yatafanyika leo Kijiji cha Mpuga Wilayani Rungwe mkoani Mbeya.
 Rafiki zake marehemu Gabriel wakiwa katika msiba huo.
 Michango mbalimbali ikipokelewa.
 Wakina mama wakiwa katika msiba huo.
 Dada zake Gabriel wakilia katika msiba huo.
 Mtoto wa kaka yake Gabriel, Helena Mathias (katikati), akilia kwa uchungu kwa kupotelewa na baba yake mdogo ambaye alikuwa ni kipenzi chake mkubwa.
 Uagaji ukiendelea.
 Ndugu jamaa na marafiki wakiwa kwenye msiba huo.
 Dada ya marehemu Elines Mwaibale (kushoto), akiwa na bibi wa marehemu wakati wa kuaga mwili huo.
 Dada wa marehemu Neema akiwa ameanguka chini baada ya kupoteza fahamu wakati wa kuaga mwili huo.
 Baba mdogo wa marehemu Kulwa Mwaibale na jirani yake na marehemu wakiweka vizuri mfuni wa jeneza baada ya shughuli ya kuaga mwili huo kukamilika.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Gabriel tayari kwa safari ya kwenda mkoani Mbeya kwa mazishi yaliyofanyika leo kijiji cha Mpuga Lutengano Tukuyu mkoani Mbeya.
Gari likiwa tayari kwa safari hiyo.

NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII

$
0
0
Kwa kipindi cha karne hii ya 21, vijana wenye umri wa chini wamekuwa watumwa wa mitandao ya kijamii, je nini hasara na faida zake?

Kumekuwa na kesi nyingi zinazoendelea kuhusu Internet Addiction Disorder( IAD), ambapo umekuwa ni ugonjwa unaokufanya usiweze kukaa au kufanya kitu bila kupitia kwenye internet, hali hii imesadikika kuweza kuangamiza kizazi kikubwa cha karne ya 21, na hasa kuleta matatizo katika mishipa ya fahamu, matatio ya kisaikolojia na ya kijamii.

Matatizo ya mishipa ya fahamu yanapelekea hata kuwa na uwezo mdogo wa kufikiria kwa haraka hasa pale unapokuwa upo makini katika kuperuzi simu yako, pia kichwa kuuma kwa muda mrefu kwa kutumia muda mwingi katika simu yako na hata baadae kuchoka kiakili na kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo .

Kisaikolojia inamuharibu kijana hasa katika uwezo wa kufikiri na kuwaza, anaweza kujihisi hawezi kukaa bila simu yake, hawezi kukaa bila kujua nani kafanya nini au afanye nini kuwaridhisha marafiki wa kurasa za facebook na Instagram, na hata kupelekea kuleta matabaka katika jamii watu kujuana kiundani na kutengeneza chuki kwa baadhi ya watu au nchi, na hata kuleta kuigana katika mtindo wa maisha.

Watu wengi wamelalamika kuhusiana na kuaibishwa kupitia mitandao ya kijamii, lakini kwa baadhi ya nchi kama Tanzania kumekuwa na sheria za kuzuia matumizi mabaya ya internet.

Lakini pia, kwa upande wake Andrea Guzzoni ambaye ni Meneja Mkazi wa kampuni ya JovagoTanzania alifafanua kuwa, Matumizi ya tovuti yanafaida kubwa kiuchumi, watanzania hawana budi kuangalia suala hili kwa upande wa pili.

“Tutumie kurasa za facebok, Instagram na Twitter katika kujifunza mambo ya kimaendeleo na kutangaza biashara zetu, lakini pia serikali inabidi iwajibike katika kuzuia baishara za utapeli zinazoendelea ndani ya mitandao” aliongezea.

“Wapo waliofanikiwa kupitia hii mitandao na wapo wanaondelea kuharibikiwa kupitia mitandao hiyo hiyo, ni wakatai wa kubadilika na kutumia uhuru wa habari kwa manufaa yetu”. Lilian Kisasa, Meneja Mawasiliano wa Jovago Tanzania aliongezea.

DR. HAMISI KIGWANGALLA AMUUNGA MKONO RAIS DKT. MAGUFULI KUPUNGUZA 2% ZA KODI KATIKA MISHAHARA

$
0
0
Dr. Hamisi Kigwangalla.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ameutangazia umma wa watanzania kuwa ameshusha kiwango cha kodi inayotozwa kwenye mshahara wa wafanyakazi wa ngazi ya chini (lower bracket) kutoka 11% mpaka 9%. Hili ni punguzo la kihistoria.

Najua malengo ya kufanya hivi ni kukidhi haja ya watumishi ya muda mrefu kuwa kiwango cha kodi kishuke kiwe 'single digit', pia kupunguza mzigo wa kodi kwa watumishi na hivyo kuwaongezea kipato chao. Pia ameweka msisitizo kwenye azma yake ya kushusha kiwango cha mshahara wa waliokuwa wanalipwa mishahara mikubwa na kuhakikisha haizidi 15mn - lengo likiwa ni kupunguza 'gap' kati ya walionacho na wasionacho kwenye nchi.

Ukimsikia Rais Magufuli anazungumzia mambo ya kuleta usawa nchini utajua wazi kabisa kuwa 'maneno yake yanatoka kwenye special corner ya moyo wake', maana anayazungumza kwa 'passion' ya hali ya juu sana kiukweli. Kwenye hili, ninamuahidi, kwa dhati kabisa, kumsaidia kutimiza hayo malengo yake kwa nguvu zangu zote, na kwa 'passion' na kasi kama ya kwake. Maana ni katika mambo ninayoyaamini na yaliyonifanya niingie Bungeni kwenye utumishi kwa wananchi, na 'passion' hiyo inatoka moyoni mwangu kabisa. Wakati natangaza nia ya kuomba nipewe ticket ya CCM kuwa mgombea wake wa uRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania niliwahi kusema kuwa 'kizazi chetu cha viongozi kisikubali tuwe na matabaka ya aina mbaya kabisa kwenye nchi yetu: kwamba, tuna kundi moja la watu wengi wanaoamka kila siku asubuhi na kutembea maili 10 kusaka mlo wa siku hiyo, huku tuna kundi lingine linalotafuta walau muda wa kutembea maili 10 ili kukata vitambi vyao!'

Somo kubwa la kujifunza hapa ni kwamba, mfanyakazi hana namna ya kukwepa kodi ya serikali ya PAYE, maana serikali anachukua kodi yake kwanza kabla mfanyakazi hajalipwa mshahara. Tofauti na wafanyabiashara, ambao wanazalisha, kisha wanaanza mambo ya makadirio ya kodi ya serikali. Niliwahi kusoma kitabu cha Robert Kiyosaki, Rich Dad - Poor Dad, anayesema kuwa 'watu wajanja hawawezi kukubali kuajiriwa, maana hawawezi kuwa tayari kukubali kukatwa kiasi kikubwa cha pesa kama kodi, wajanja hujiajiri wenyewe kwa kuwekeza na kuzungusha mitaji kutafuta faida kisha kutafuta kila namna ya kukwepa kodi ya serikali, na hivyo kundi hili la pili huishi maisha ya raha kwa kuwa lina uhakika wa kutajirika.'

Kwa vijana wa nchi yetu wanaohangaika kutafuta ajira siku hata siku wana la kujifunza hapa. Kama wanataka mali, watayapata shambani.

MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA), YAAZIMISHA SHEREHE ZA KODI JIJINI DAR ES SALAA

$
0
0
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Victor Kimaro (wa kwanza kushoto) akizugumza na wadau mbalimbali (hawapo pichani) juu ya uwezo wao wa kumudu ukusanyaji wa kodi vizuri ili waweze kufanikisha vizuri malengo waliyo jiwekea mwaka huu. Pia aliwashukuru (ITA) kwa kujitolea kutoa elimu kwa wawekezaji wote wanaofika hapa nchini iliwaweze kulipa kodi wanapo wekekeza hapa nchini. alizungumza hayo Siku ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016
02.Mdau akifafanua jambo kwenye sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 201
Sehemu ya wadau mbalimbali waliohudhuria hizo wakimsikiliza Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Victor Kimaro kwenye sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016

TANZANIA BLOGGERS NETWORK (TBN) WAADHIMISHA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI KWA KUPINGA KUBAGULIWA

$
0
0
 Chama cha Wamiliki/Waendeshaji wa Mitandao ya Jamii nchini 'Tanzania Bloggers Network'– TBN inawaomba wanachama wake wote kutotumia taarifa ama habari au picha yoyote kutoka katika mkutano wa maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari (WPFD) unaofanyika kitaifa mkoani Mwanza.

Kamati Kuu ya Uongozi TBN imefikia hatua hiyo leo baada ya kujadiliana na kujiridhisha kuwa kumekuwepo na taasisi za tasnia ya habari ambazo zimekuwa zikiwatenga wanahabari wa mitandao ya kijamii (bloggers) na kutotambua umuhimu wao wakati sehemu kubwa ya taarifa mbalimbali nchini husambazwa na mitandao hiyo.

TBN iliyosajiliwa rasmi serikalini Aprili 2015 na kupewa namba ya usajili; S. A 20008 inawataka wanachama wake kutotoa ushirikiano wa sina yoyote kwa taasisi ambazo zinawatenga bloggers.

Tunasikitika kufikia hatua hii ila hamna jinsi. TBN itasikitika na kumshangaa mwanachama wake au blogger asiye mwanachama kutounga mkono agizo hili, na kwenda kinyume na agizo hili. Muda umefika ‘Bloggers’ kudai heshima, kutambulika na kuthaminika kama tasnia ya habari nyingine yoyote.

Imetolewa na;-
Mwenyekiti wa Muda wa TBN
Joachim E. Mushi
03/05/2016

KUTANA NA ‘GREEN VOICES’, SAUTI ZA AKINAMAMA WAPAMBANAO NA MABADILIKO YA TABIANCHI

$
0
0
Akinamama wanaoshiriki katika mradi wa kupaza sauti za wanawake wanaopambana na mabdiliko ya tabianchi – Green Vocies katika picha ya pamoja na viongozi wa Foundation For Women of Africa na wafadhili wa mradi huo, mara baada ya uzinduzi wa mradi huo Madrid, Spain hivi karibuni.
Mama Maria Tereza (katikati) - Rais wa taasisi ya Foundation for Women of Africa akiwa na waandishi wa habari wanaotekelza mradi wa Green Voices wakati wa hafla ya kuwakaribisha kinamama nchini Spain. Kutoka kushoto ni Secelela Balisidya, Tukuswiga Mwaisumbe, Farida Hamis, Siddy Mgumia na aliyechuchumaa Judica Losai.
Akinamama wanaoshiriki katika mradi wa kupaza sauti za wanawake wanaopambana na mabdiliko ya tabianchi – Green Vocies katika picha ya pamoja na uongozi wa chuo kikuu cha Universitad Automous De Madrid, mara baada ya kutembelea mazingira ya chuo hicho Madrid, Spain hivi karibuni.
Ziara ya mafunzo kujifunza jinsi ya kutengeneza mbolea ya mboji.
Ziara ya mafunzo kujifunza majiko yanayotumia nishati ya jua.
Ziara ya mafunzo katika chumbancha habari cha gazeti la El Pais.
Akimama na wawezeshaji wa mafunzo katika picha ya pamoja darasani.---
WANAWAKE wapatao 15 hivi karibuni walihudhuria mafunzo ya kuongeza ujuzi wa jinsi ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi nchini Spain. Mafunzo na mradi huo vinafadhiliwa na Taasisi inayojihusisha na maendeleo ya wanawake wa Afrika, ijulikanayo kama Foundation for Women of Africa inayoongozwa na Makamu wa Rais mstaafu waSpain Mama María Teresa Fernández de laVega.
---
Taasisi hiyo itafanya kazi na wanawake hao 15 wa kitanzania kupitia miradi inayosaidia nchi kupambana na mabadiliko ya tabianchi. Wanawake hao ambao kati yao watano ni waandishi wa habari kila mmoja atatekeleza mradi mmoja, huku waandishi wa habari wakisaidia kupaza sauti za akinamama hao kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Mradi huu unaojulikana kama GREEN VOICES una lengo la kupaza sauti za akinamama kueneza ujuzi wao wa kupambana na mabadiliko ya tabianchi ili jamii nzima ya kitanzania iweze kujifunza zaidi na kuzitumia mbinu hizo katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Mradi huo unaoratibiwa hapa nchini na Mtandao wa wanahabari wa Mazingira (EMNet) kwa niaba ya Foundation for Women of Africa unatekelezwa katika mikoa sita ya Kigoma, Kilimanjaro, Mwanza, Morogoro, Dar es Salaam na Pwani ukihusisha miradi ya kilimo, usindikaji, ufugaji na utafiti.

Mratibu wa EMNet Secelela Balisidya amesema akinamama hao wanatekeleza miradi ambayo inachangia moja kwa moja aidha kupambana au kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesema miradi hiyo ni mradi wa kilimo cha miti ya matunda mkoani Kigoma, kilimo cha viazi lishe visiwani Ukerewe mkoani Mwanza, Ufugaji Nyuki mkoani Morogoro na Pwani na ukaushaji wa mbogamboga kwa kutumia nishati ya jua mkoani Morogoro. Miradi mingine ni usindikaji wa vyakula mbalimbali kutokana na muhogo mkoani Pwani, kilimo hai cha mbogamboga na kilimo cha uyoga mkoani Dar es Salaam, mradi wa majiko banifu mkoani Pwani na mradi wa utafiti wa jiko linalotumia nishati ya jua mkoani Kilimanajro.

Mradi huo unaotarajiwa kutelekezwa kwa mwaka mmoja unatoa fursa kwa kinamama kutoa ujuzo wao wa kupambana na mabadiliko ya tabianchi na sauti zao kusikika. Hiyo ni kwa sabuabu kinamama wana uhusiano mkubwa na mazingira kutokana na kazi wanazozifanya kila siku za kilimo na utunzaji wa familia kuhusiana moja kwa moja na mazingira hivyo kuyaelewa zaidi mazingira na jinsi ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Wakiwa Madrid nchini Spain walikopata mafunzo wa wiki mbili katika chuo kikuu cha Autonomus Universitad De Madrid, akinamama hao na waandishi wa habari walijifunza kwa nadharia na vitendo jinsi nchi ya Spain inavyokabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kuona njia ambazo na huku nchini zinaweza kutumika kupambana na mabadiliko ya tabianchi. Mafunzo kwa vitendo pia yalihusisha ziara za mafunzo kujifunza kilimo hai, na jinsi nishati jua inavyoweza kusaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Waandishi wa habari pia walipata nafasi ya kutembelea chumba cha habari cha gazeti la Serikali ya Sapin la El Pais an kujifunza zaidi jinsi waandishi wa huko wanavyoandika habari zihusianazo na mabadiliko ya tabianchi.

UBALOZI WA DENMARK KUENDESHA MDAHALO KUHUSU AFYA NA HAKI ZA WANAWAKE NA WASICHANA, TAREHE 05 MEI, 2016

$
0
0
 Ubalozi wa Denmark nchini kwa kushirikiana na shirika la Marie Stopes Tanzania – MST, Femina Hip; Msichana Initiative; pamoja na wizara ya afya, ustawi wa jamii, jinsia wazee na watoto, wameandaa kongamano kuhusu afya, haki na uwezeshaji wa wanawake litakalofanyika kesho Alhamis May 05, 2016.

Kongamano hilo ambalo ni sehemu ya maandalizi ya kongamano la kimataifa ambalo mwaka huu litafanyika mjini Copenhagen, Denmark baadaye mwezi huu, litafanyika kwenye Makumbusho ya taifa jijini Dar es salaam; mada kuu ikiwa ni kwa jinsi gani Tanzania itaweza kufikia malengo endelevu ya milenia kwa wanawake na wasichana ifikapo mwaka 2030.

Kongamano la Copenhagen litakalofanyika kuanzia May 16 hadi 19 mwezi huu, ni kongamano kubwa zaidi la kimataifa linalolenga masuala ya afya, haki, usalama na uwezeshaji wa wanawake na wasichana. Mada kuu ya mwaka huu itakuwa ni utekelezaji wa Malengo mapya ya maendeleo endelevu – SDGs ambayo yaliwekwa na mkutano mkuu wa umoja wa Mataifa Agosti, 2015.

Lengo la mdahalo wa kesho ni kujadili kwa uwazi jinsi Tanzania itavyoweza kufanikiwa kufikia matarajio ya malengo ya maendele endelevu, yanayohusiana na wanawake na wasichana hususani afya ya uzazi na haki zao katika masuala ya usawa wa kijinsia, elimu, mazingira na uwezeshwaji wa kiuchumi.

Mdahalo huu wa wazi utaongozwa na Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu, pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TACAIDS, Fatma Mrisho; Mkurugenzi mkuu wa Chama cha wanasheria wanawake Tanzania, Tike Mwambipile, na Mkurugenzi wa huduma za afya wa shirika la Marie Stopes Tanzania Mwemezi Ngemera.

Mdahalo huo pia utawesha kubaini vipaumbele vya utekeleza kwa Tanzania kuweza kufikia malengo ya maendeleo endelevu yanayohusiana na wanawake na wasichana ili kutambua na kudhamini mchango wao katika jitihada za Tanzania kufikia maendeleo endelevu.

Mdahalo huu pia utaambatana na maaonesho ya shughuli mbalimbali za kuhamasisha afya na haki kwa wanawake na wasichana.

TIGO 4G LTE YAINGIA KWENYE MIJI 5 KANDA YA ZIWA

$
0
0
Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mpango wa Tigo kusambaza mtandao wa 4G lte nchi nzima pembeni yake ni Afisa Mkuu wa Ufundi wa teknolojia ya mawasiliano wa Tigo Jerome Albou katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika ofisi za makao makuu ya Tigo Kijitonyama Jijini Dar es salaam.
Waandishi wa habari wakichukua taaarifa
Mtandao wa Tigo 4G LTE ni mpana na wa kasi Tanzania
 
Kampuni ya simu ya Tigo ambayo
inaendesha maisha ya kidijitali Tanzania imetangaza kuzinduliwa kwa huduma ya 4G LTE katika miji mingine mitano ya kanda ya ambayo ni Tabora, Musoma, Bukoba, Kigoma na Shinyanga.

Kampuni hiyo awali ilizindua huduma hiyo jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa mwaka jana na baadaye kuisambaza katika miji ya Arusha, Tanga, Dodoma, Morogoro, Moshi na Mwanza na hivyo kuifanya kuwa kampuni ya simu yenye mtandao mpana na wa kasi wa 4G LTE nchini Tanzania.

Ikiwa inachukuliwa kuwa ni teknolojia nzuri na ya uhakika katika sekta ya mawasiliano ya
simu duniani ya kupata intaneti, kasi ya teknolojia ya 4G LTE ni takribani mara tano zaidi ya teknolojia ya 3G na Tigo inaifanyia kazi kwa kina ili kuongeza ubora wa huduma hiyo na mtandao wa 4G kutokana na matumizi ya wateja kuwa nayo yanaongezeka kwa kasi kubwa.

Hivi sasa Tigo ina timu inayofanya kazi saa zote kuimarisha na
kukuza ubora wa teknolojia ya 4G. Matokeo yake ni kwamba mtandao wa 4G umekuwa unategemewa kwenye miji ambamo upo (Arusha, Tanga, Dodoma,
Morogoro, Moshi na Mwanza).

Mtandao wa 4G LTE unatoa intaneti ya kasi ya kurambaza (surf) na kupakua vitu, kufanya miito ya simu ya kuonana (Skype) isiyo na kikomo. Kutokana na uzinduzi wa hivi karibuni wa video za bure kupitia YouTube nyakati za usiku, mtandao wa 4G LTE unawawezesha wateja kwa
kiwango kikubwa kupata uzoefu wa
kutiririsha video zilizo na uangavu mkubwa. Aidha kutokana na ushirikiano na Facebook mteja wetu wa 4G pia anaweza kufurahia kutiririsha video zilizomo kwenye mitandao maarufu ya kijamii duniani.

Pia, mteja akiwa na 4G LTE anaweza kupakua mafaili makubwa (sinema, mafaili yanayohusiana na kazi) au vifaa na hali kadhalika kucheza michezo kwa njia ya mtandao.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez, alisema mpango wa kupanua teknolojia ya 4G hadi kwenye maeneo yote ya nchi upo mbioni ambapo kampuni hiyo imejikita kwenye kuwapa wateja wake hudumazenye ubora duniani ambazo zitawawezesha kufurahia mtindo wa maisha ya kidijitali.

“Kupanua mtandao wa 4G LTE nchi nnzima kwa mara nyingine kunaonesha sio tu Tigo
kuongoza kwenye kutoa teknolojia na ubunifu wa kisasa ndani ya soko bali pia kusisitizia kujituma kwetu katika kuongeza fursa ya kufikia intaneti kwa Watanzania walio wengi kwa kadri iwezekanavyo,’ alisema Gutierrez.

Kwa mwaka huu 2016, Tigo itawekeza zaidi ya dola milioni 75 kwenye upanuzi wa mtandao na kuimarisha ubora wake kwa kukuza maeneo ya teknolojia ya 4G na 3G, mkongo wa mawasiliano na hali kadhalika kuongeza idadi ya sehemu za kutolea huduma kwa wateja nchi nzima.

“Tukiwa kama kampuni tunatambua umuhimu wa wa ubora na ukaribu kwa wateja wetu na tunafanya kazi ili kufikia malengo hayo katika siku za karibuni,” alisema Gutierrez.

“Hivi sasa pia tuna programu ya kufanya mtandao kuwa wa kisasa ambao unajumuisha kuongeza uwezo wa 4G kwenye miji yote 12 ambako tuna mtandao wa 4G pamoja na kuongeza mtandao wa 3G kufika maeneo yote nchini,”alisema Gutierrez na kuongeza kuwa wateja wa Tigo katika miji ya Mbeya, Mtwara na Lindi wajitayarishe kufurahia huduma ya Tigo 4G LTE itakayoanza kutolewa siku za hivi karibuni.

WATOTO OMBAOMBA JIJINI MWANZA WABUNI NJIA YA KUJIPATIA KIPATO

$
0
0
Watoto wanaoishi Mitaani Jijini Mwanza wakiwa katika shughuli ya kufuta magari na kuomba pesa.

Wanapitia wakati mgumu Mitaani. Wanakosa malezi bora na fursa muhimu kama vile kupata elimu. Hakika wanahitaji mpango mkakati ili kunusuru ndoto zao ambazo zinapotelea mitaani. Wapo wenye ndoto za kuwa Wachezaji bora duniani, watangazaji na waandishi bora wa habari, waalimu na taaluma nyingine kede wa kede. Swali ni je; ndoto hizo zitatimia vipi?

Nawazungumzia Watoto wanaoishi Mitaani ambao wamekuwa wakionekana katika Miji na Majiji mbalimbali hapa nchini ikwemo Jijini Mwanza, wakirandaranda mitaani na hata kuishi mitaani.

Wana makwao, japo ukiwauliza kwa nini wamekimbilia mitaani, wanasema wametoroka mateso na manyanyaso kutoka kwa ndugu na walezi wao baada ya wazazi kufariki ama kutengana katika ndoa.

Wachache pia wamekuwa wakitumiwa na wazazi ama walezi wao kama sehemu ya familia kujipatia kipato kupitia shughuli ya kuombaomba mitaani.

Jijini Mwanza kasi ya ongezeko la Watoto wa Mitaani inazidi kuongezeka maradufu. Jamii mara kadhaa imekuwa ikihimizwa kutowapa watoto hao pesa kwa kuwa hali hiyo huwafanya kuona maisha ya mitaani ni matamu zaidi. Lakini hiyo si hoja tena, watoto hao sasa wamebuni njia ya kujipatia kipato ambapo wengi wao hukaa eneo la Mataa, Nyerere Road na kufanya shughuli ya kusafisha na kufuta vuti katika magari kwa minajiri ya kupata kipato.

Binagi Blog inashauri, Mkakati zaidi ufanyike ili kunusuru vipaji vya watoto hawa walio mitaani. Watoto hawa wana makwao, wakamatwe na kurudishwa walikotoka, ikishindikana katika hilo, vituo vya kulelea watoto hao vitimize wajibu wa kuwalea. Mwisho kabisa, Magereza za watoto zitumike kuwapa malezi wale watakaoonekana kichwa ngumu katika kutii moja ya mkakati utakaokuwa umepewa kipaumbele katika utekelezaji.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AAGANA NA BALOZI CHIKAWE, AKUTANA NA BALOZI WA DENMARK

$
0
0

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi MathiasChikawe ambaye ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania nchini Japan Balozi Chikawealipofika  kumuaga Waziri Mkuu ofisinikwake mjini Dodoma leo akiwa tayari kwenda kuanza kazi yake.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi waDenmark nchini Tanzania Bwana Einar Jensen ambaye alifika ofisini kwa wazirimkuu mjiniDodoma kwa mazungumzo ya kikazi.Picha na Chris Mfinanga.

VYOMBO VYA HABARI VYA MAGAZETI CHALI DHIDI YA DIGITALI

$
0
0

Vyombo vya habari vya asilia hususan magazeti vinakufa. Hivi sasa vvyombo hivyo vinajikongoja kutokana na  mauzo hafifu  na mdororo wa mapato kutoka matangazo na kupunguza wafanyakazi.
Ila wakati idadi ya wasomaji wa habari mtandaoni ikizidi kukua, wanaoperuzi mtandaoni  humo hawatumii muda mwingi kwenye magazeti tando, utafiti wa Pew Research Centre unaeleza. 

Katika utafiti wake wa hali ya vyombo vya habari 2015 ("State of the News Media 2015,”) imeonesha kwamba katika vyombo vya habari vya karatasi (print media), Digitali na TV, imeonesha Dhahiri kwamba magazeti yanaelekea kuzimu.
Utafiti huo umetolea mfano magazeti makubwa ambapo wasomaji wake wa mtandaoni wamewashinda kwa mbali kwa idadi ya wasomaji wa makaratasini, ambapo gazeti kubwa sana la New York Times la Marekani limetangaza kuwa nakala zake zipatazo 650,000 kwa wiki zimepitwa kwa mbali sana na wa mitandaoni.
 Hivi sasa kuna mjadala mitandaoni endapo kama Tanzania iko ama itafika huko. Mabishano ni makali ambapo wa makaratasini wanashikilia msimamo wao kuwa nchini hapa tasni ya habari mtandaoni bado ni change sana kuweza kutishia amani ya magazeti. 
Upande wa digitali unajibu kwamba endapo kama kuna wahariri viburi wanaobeza kasi ya mitandao, basi wakae mkao wa kulala njaa muda si mrefu ujao, maana ni wachache wanaoendelea kupata habari kwa njia asili ya magazeti. 
Upande wa digitali umeyasifia magazeti ya Global Publishers na la Mwananchi  ambayo ni dhahiri yana wahariri wanaokwenda na wakati na wanaojua nini wanachokifanya kwa kuanza na mapema kuogelea bahari ya maendeleo ya tasnia kwa vitendo kwa kuwa na vitengo vya mtandao vinavyopelekesha mbio magazeti yanayobeza technolojia hiyo kwa kubuni.

"Ni kweli kwamba Tanzania ni bado sana kiteknolojia na miundombinu kiasi cha habari za mtandaoni zikatishia uhai wa habari za makaratasini, lakini si uwongo kwamba ukizingatia uharaka na gharama pamoja na kwenda na wakati muda si mrefu print media itakwenda na maji", amesema blogger mmoja ambaye pia ni mwanahabari kwenye moja ya magazeti makubwa nchini.

BEI YA WESE YAPANDA

$
0
0

TANAPA KUBADILI MFUMO WA UTENDAJI KAZI KUTOKA KIRAIA KUWA JESHI USU

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA) Allan Kijazi (kulia) akimuongoza Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi kuelekea katika uwanja wa Mafunzo katika kambi ya Mlele kwa ajili ya kufunga Mafunzo ya Wahifadhi na Askari wapya waajiriwa wa shirika hilo .
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi akipiga saluti wakati akipokea salamu za heshima wakati wa gwaride maalumu la ufungaji wa mafunzo ya awamu ya mabadiliko ya mfumo wa utendaji kazi wa kiraia kuwa mfumo wa jeshi usu.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi akikagua gwaride la heshima la askari wapya na Wahifadhi waliohitimu mafunzo ya awamu ya kwanza ya mabadiliko ya mfumo wa utendaji kazi wa kiraia kuwa mfumo wa jeshi usu yaliyofanyika katika kituo cha mafunzo Mlele mkoani Katavi.
Askari waajiriwa wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) kwa mwendo wa pole na kutoa heshima wakati ufungaji wa mafunzo ya mfumo wa jeshi usu kwa Wahifadhi
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi akipiga saluti wakati gwarde likipita mbele ya jukwaa na kutoa heshima,wengine kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Wanyamapori, Martin Loibooki,Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali Mstaafu, Raphael Muhuga, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa, Allan Kijazi, Kaimu Mkurugenzi idara ya Wanyama pori, Ndugu Karamaga.
Askari waajiriwa wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) kwa mwendo wa haraka wakati ufungaji wa mafunzo ya mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi
Askari wapya waajiriwa wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakionesha umahiri katika kutumia silaha wakati wa kukabiliana na majangili mara baada ya kupata mafunzo hayo katika kambi ya Mlele iliyopo mkoani Katavi. 
Baaadhi ya Wahifadhi Waandamizi na Wafawidhi wakiwa wameshika silaha mara baada ya kupatiwa Mafunzo katika Kambi ya Mlele ikiwa ni sehemu ya mabadiliko ya mfumo wa utendaji kazi wa kiraia kwenda Jeshi Usu. 
Askari wa Hifadhi akionesha umahiri katika matumizi ya silaha kwa kulenga shabaha wakati wa kuhitimu mafunzo ya  awamu ya kwanza ya mabadiliko ya mfumo  wa utendaji kazi wa kiraia kuwa mfumo wa jeshi usu yaliyofanyika katika kituo cha mafunzo Mlele mkoani Katavi
Baadhi ya Viongozi na Wageni katika hafla ya ufungaji wa Mafunzo ya Mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi na askari waajiriwa wakifuatilia maonesho yaliyokuwa yakifanywa na wahitimu hao.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete (kulia) akiratibu shughuli mbalimbali zilizokuwa zikiendelea katika hafla ya ya ufungaji wa Mafunzo ya Mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi na Asakari Waajiriwa .kushoto ni Mkuu wa Mafunzo ,Genes Shayo .
Mhifadhi Sekela
Mwangota akisoma risala  ya Wahitimu wa
Mafunzo ya Mfumo wa Jeshi Usu kwa mgeni rasmi ,Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili
na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi (hayupo pichani) wakati wa kuhitimisha
mafunzo hayo kwa wahifadhi na askari wapya waaajiriwa wa shirika la Hifadhi za Taifa
(TANAPA) yaliyofanyika kwenye kambi ya Mafunzo Mlele mkoani Katavi.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Wanyamapori,Martin Loibooki akizungumza wakati wa hafla ya ya ufungaji wa Mafunzo ya Mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi na Asakari Waajiriwa .
Baadhi ya Wahitimu.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akizungumza wakati waa hafla ya ya ufungaji wa mafunzo ya mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi na Askari Waajiriwa .
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Meja Jenerali Mstaafu ,Raphael Muhuga akizungumza hafla ya ya ufungaji wa Mafunzo ya Mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi na Askari Waajiriwa ambapo amegusia juu ya changamoto iliyopo kwa Wafugaji kuingiza Mifugo yao katika Hifadhi pamoja na mapori ya Akiba.
Katibu Mkuu ,Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi akitoa hotuba yake ya kuhitimisha Mafunzo ya Mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi na Askari waajiriwa wa Shirika la Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA),Mafunzo yaliyofanyika katika kambi ya Mlele mkoani Katavi.
Baadhi ya Askari Waliohitimu.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi akitunuku vyeti kwa Wahitimu wa Mafunzo ya Mfumo wa Jeshi Usu kwa Wahifadhi za Taifa(TANAPA) yaliyofanyika kambi ya mafunzo Mlele mkoani Katavi.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini aliyeko Katavi.

RAIS MSTAAFU, JAKAYA KIKWETE ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO UBALOZI WA KENYA

$
0
0

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliyeambatana na Mkewe, Mama Salma Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Kenya hapa nchinikufuatia kifo cha Mke wa Rais Mstaafu wa Kenya, Mhe. Nwai Kibaki, Mama Lucy Kibaki kilichotokea wiki iliyopita nchini Uingereza. Mwingine katika picha ni Naibu Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Boniface Muhia. Dkt. Kikwete anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwenye mazishi ya Mama Kibaki yatakayofanyika Nairobi, Kenya.
Mama Salama Kikwete naye akisaini Kitabu cha Maombolezo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje,Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Dkt. Aziz Mlima naye akisaini kitabu cha maombolezo.
Rais Mstaafu, Dkt. Kikwete (wa pili kutoka kushoto) akimsikiliza Naibu Balozi, Mhe. Boniface Muhia (wa pili kutoka kulia), mara baada ya kumaliza kusaini kitabu cha maombolezo, Mama Salama Kikwete (wa kwanza kushoto) na Balozi Mlima nao wakimsikiliza Naibu BaloziPicha na Reginald Philip.

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AMUAPISHA DKT. ASHA-ROSE MIGIRO KUWA BALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Asha-Rose Migiro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza katika Ikulu ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Dkt. Asha-Rose Migiro mara baada ya kumuapisha kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza katika Ikulu ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Dkt. Asha-Rose Migiro Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Dkt. Asha-Rose Migiro Balozi wa Tanzania nchini Uingereza pamoja na Profesa Cleophas Migiro mme wa Dkt. Asha-Rose mara baada ya tukio la uapisho katika Ikulu ndogo ya Chwamwino mkoani Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Dkt. Asha-Rose Migiro Balozi wa Tanzania nchini Uingereza huku Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Augustine Mahiga wakisikiliza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mara baada ya kutoka kwenye tukio la kumuapisha Dkt. Asha-Rose Migiro kuwa Balozi mpya nchini Uingereza . PICHA NA IKULU.
---
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza.

Hafla ya kuapishwa kwa Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro imefanyika leo tarehe 05 Mei, 2016 katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma, na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Peter Kallaghe ambaye amerudishwa nyumbani.

Akizungumza baada ya kuapishwa, Dkt. Migiro ameahidi utumishi uliotukuka na kwamba atahakikisha uhusiano na ushirikiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Uingereza unaimarishwa zaidi, hususani katika kuvutia uwekezaji, biashara na utalii baina ya nchi hizi mbili.

Dkt. Migiro pia ametoa wito kwa watanzania waliopo hapa nchini na waishio Uingereza kuitumia ofisi hiyo ya ubalozi ipasavyo, ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali hasa za kiuchumi.

TIMU YA MENEJIMENTI YA NHC NCHI NZIMA YATEMBELEA MIRADI YA SHIRIKA HILO JIJINI DAR

$
0
0
1 
Meneja Mradi wa Shirika la nyumba la Taifa NHC Kawe jijini Dar es Salaam unaokwenda kwa jina la 711 Injinia Samwel Metil akitoa maelezo kwa Timu ya Menejimenti ya NHC wote (Directors, Regional Managers & Line Managers) wakati walipotembelea miradi ya 711 Kawe, Morocco Square, Victoria Place, Eco Residence na Kibada ambapo ambapo pia watafanya pia kazi katiia miradi hiyo Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kuwafahamisha juu ya maendeleo na changamoto za miradi hiyo.
2
Mmoja wa Mainjinia wa Mradi wa 711 Kawe Bw. Kishor Hirani akimelezea jambo Meneja mradi Injinia Samwel Metil wakati menejimenti ya shirika hilo ilipotembelea katika mradi huo.
3
Wakuu wa vitengo mbalimbali na mameneja wa mikoa wakitembelea mradi wa 711 Kawe leo.
4
Mmoja wa Mameneja wa NHC kutoka mkoani Dodoma Bw. Itandula Gambalagi pamoja na wenzake wakiwasili kutembelea mradi wa Morocco Square.
56Wakipatiwa maelezo katika mradi wa Morocco Square.
7 
Mameneja hao wakifuatilia maelezo ya mradi wa Morocco Square.
8
Muungano Saguya kulia Yahya Charahani kushoti na Itandula Gambalagi wakijadiliana jambo wakati walipotembelea mradi wa 711 Kawe jijini Dar es Salaam pamoja na wenzao.
9
Jengo la Mradi wa Eco Residents ambalo limekamilika kwa asilimia 99%.
11 
Ujenzi wa mradi wa 711 Kawe ukiendelea.

MAMIA WAMZIKA ANDREW NICKY SANGA (KING DREW) DODOMA

$
0
0
Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga Enzi za Uhai wake
Mwili wa Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga (King Drew) ukiwa unawasili katika uwanja wa Mashujaa kwa ajili ya Ibada na Kutoa kutoa Heshima za mwisho
Ibada ikiwa inaanza Baada ya Mwili wa Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga kuwasili
 Kwaya wakiwa wanaimba wimbo wao wakati wa kujiandaa na ibada
Familia,Ndugu wa karibu, pamoja na Viongozi Mbalimbali wa Serikali wakiwa katika ibada ya kumsindikiza Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga
Mmoja wa Marafiki wakubwa wa Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga Victor Mponzi akiwa anasoma Historia na wasifu wa Marehemu.
Mmoja wa Marafiki wakubwa wa Marehemu Andrew Nicky Sanga akiwa anatambulisha  wageni.
Huyu ni Rafiki yake sana na Marehemu Andrew Nicky Sanga ambaye anatoka Marekani na alikuja pamoja na Mwili akitoa salamu zake za Rambirambi kutoka Houston
Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma akitoa salamu zake za rambirambi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa.
Mbunge wa Mbeya Mjini Mh. Joseph Mbilinyi akiwa anatoa salamu za Rambirambi na kueleza namna alivyo mfahamu Marehemu Andrew Nicky Sanga
Mh. Mbunge wa Viti maalum akitoa salam za rambirambi na kusisitiza upendo kama aliokuwa nao mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga
Baba Askofu wa Dayosisi ya Central Tanganyika Dkt. Dickson Chilongani akitoa neno la Mungu la wakati wa Ibada ya kuaga Mwili wa Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga.
 Ndugu ,Jamaa na Marafiki wakiwa katika ibada ya Mazishi ya  mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga uwanja wa Mashujaa.
 Baba wa Mzazi mwenzake na Marehemu Andrew Nicky Sanga akitoa heshima za mwisho
 Mbunge wa Mikumi Mh. Joseph Haule akitoa Heshima za mwisho
 Baba wa Marehemu Andrew Nicky Sanga akitoa heshima zake za mwisho kwa mwanae mpendwa
 Mzazi mwenzake na Marehemu Andrew Nicky Sanga akiwa na Mtoto wao mpendwa Zoe wakitoa heshima zao za mwisho.
Watumishi wa Mungu wakiongozwa na Baba Askofu wa Dayosisi ya Central Tanganyika Dkt. Dickson Chilongani  wakitoa neno la Baraka kwa Marehemu Andrew Nicky Sanga

 Marafiki wakubwa wa Marehemu Andrew Nicky Sanga wakitoa Heshima zao za mwisho
 Msafara ukielekea Makaburini
 Mwili wa Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga ukihifadhiwa katika nyumba yake ya Milele
 Umati wa watu wakiwa Makaburini kwa ajili ya Mazishi
 Mh. Joseph Mbilinyi na Mh. Joseph Haule wakiwa Pamoja na Marafiki wengine wa Marehemu Andrew Sanga wakiwa Makaburini.
Mama mzazi wa Marehemu Andrew Nick Sanga akiwa anaweka Shada la Maua
 Baba Mzazi wa Marehemu Andrew Nicky Sanga na Mke wake wakiwa wanaweka Shada la maua
 Mtoto wa Marehemu Andrew Nicky Sanga wa katikati akiwa anaweka Shada la Maua
 Mzazi Mwenzake na Marehemu Andrew Nicky Sanga akiwa anaweka Shada la Maua
 Victor Luvena akiendelea kusoma utaratibu wa kuweka mashada
 Wazazi wa Mzazi mwenzake na Andrew Nicky Sanga wakiweka Shada.
 Wadogo zake na Marehemu wakiweka Shada la Maua
 Mh. Joseph Mbilinyi akiweka Shada la Maua
 Marafiki wa mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga waliokuja na Mwili kutoka Marekani wakiweka shada la Maua
 Marafiki wakubwa wa Marehemu Andrew Nicky Sanga wakiweka shada lao
 Baba Askofu wa Dayosisi ya Central Tanganyika Dkt. Dickson Chilongani akiweka Shada.
 Dkt. Sanga akitoa salamu za Shukurani kwa niaba ya Familia.
 Baba Askofu wa Dayosisi ya Central Tanganyika Dkt. Dickson Chilongani akisoma neno la kufunga ibada.

 Marafiki wa Andrew Nicky Sanga wakiwa katika Picha ya Pamoja baada ya Mazishi.
Kaburi la Marehemu mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga Baada ya Mazishi. Picha zote na Fredy Njeje.
Viewing all 11654 articles
Browse latest View live